SIMBU AMBAYE NI BINGWA WA MBIO ZA DUNIA AWASILI NCHINI*


Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bi. Neema Msitha, ameongoza mapokezi ya Mwanariadha Sajini Alphonce Simbu ambaye ni Bingwa wa mbio za  Dunia kwa Wanaume na mshindi wa  Medali ya Dhahabu, aliyewasili nchini alfajiri ya Septemba 23, 2025 akitokea Tokyo Japan alikoshiriki mbio hizo.

Mapokezi hayo pia yamehudhuriwa na baadhi ya Viongozi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Shirikisho la Riadha  Tanzania (RT) pamoja na familia yake.




 

Post a Comment

Previous Post Next Post