Watanzania hatutaki kudanganywa – TLP

  

Na Mwandishi Wetu

Makamu Mwenyekiti Taifa Chama cha Tanzania Labour Party (TLP), Dominata Rwechungura amesema Watanzania hawataendelea kukubali kudanganywa na wanasiasa kwa kuwa mambo yanayofanywa na serikali iliyopo madarakani yapo dhahiri.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Rwechungura alisema wameamua kutuma ujumbe kwa Watanzania wote kuwa wakatae kudandanganywa na wachambue maneno wanayoelezwa na wanasiasa wasioitaka mema nchi.

“Tunaongea na Watanzania wote, wafanyakazi, wakulima na hata watoto wa shule za awali maana TLP chama chetu kinagusa maslahi ya nchi, kuna baadhi ya wagombea urais wamechukua fomu wamejinadi na kuteuliwa tunashitushwa na kauli zao,” alisema Rwechungura na kuongeza:

“Kauli zao zinatupa ukakasi kama Watanzania kauli zao zina mashaka, zinaonyesha kuvunja amani ya taifa, zinaonyesha kutugawa, si za kweli. Mfano mtu unasema endapo sitashinda sitakubali kumuachia Mungu maana yake utafanya vurugu nchi haitatawalika watu watapigwa, watasambaratika, wafanyabiashara watapoteza vitu, utavunja amani ya nchi watu hawataenda msikitini wala kanisani.”

Alibainisha, TLP wanaye mgombea urais na wao ndio wa kwanza kufanya mkutano mkuu, Mei 9, 2020: “Tulijiridhisha kazi zote zilizofanywa na Rais Dk. John Magufuli, tukaangalia na ilani yetu ya uchaguzi uliopita, tuliahidi kusomesha wanafunzi bure, tutajega hospitali tutajenga barabara, tukasema tukichukua serikali tutahamia Dodoma ili kupunguza matumizi yafedha za walipa kodi.

“Yale yote tuliyoainisha kwenye ilani yametekelezwa na Mtanzania mwenzetu, ndugu yetu Dk. Magufuli tofauti yetu ni itikadi ya chama kila mmoja ana katiba yake, yeye ana CCM yake mimi nina TLP yangu.”

Alisema, Tanzania imepata mtu mchapakazi, msema kweli anayeletea maendeleo je wamkatae? Kila alichokifanya kinatumiwa na wapinzani na wana CCM, sasa wanamchukia kwa sababu gani: “Watu wanakwambia aliyekupenda mpende, Dk.Magufuli ametupenda sote,” alisema na kubainisha:

“Sisi mgombea wetu nawatangazia leo (jana) ni Dk. John Magufuli mzaliwa wa Chato, Mtanzania mwenzetu, tutampata wapi rais wa Watanzania atakayesimama katika kipindi cha majanga kama Corona, nchi nyingine wamekufa wengi lakini Rais Magufuliamesimama na sisi awaokoe Watanzania wake akatutaka tuombe kwa Mungu kwa siku tatu.

“Hatuwezi kukubali kuona Rais Magufuli akipakwa matope, tunawaomba wagombea urasi wanapotoa taarifa zao wafanye utafiti kila kitu kipo wazi kwenye tovuti za taasisi za umma, kwa kuwa Watanzani wa sasa si wa zamani wanajua huyu amesema uongo huyu amesema kweli.

“Usikurupuke kutoa data za uongo, mtu ana chuki zake anazichanganya na siasa unamuona hadi sura imembadilika kwa chuki zake, kataeni tumesituka TLP tumeanza kuwapima wote tumechukua kauli zao tunaona mbona kauli hii si ya uzalendo mbiona inatuletea shida, jinadi sema hoja zako jenga hoja kwa hoja watananzania wakuelewe.”

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Vijana Taifa TLP Ivan Maganza, alisema chama hicho kimeamua kumuunga mkono Rais Magufuli kwa kuwa vijana wanao wajibu kueleza umma namna mambo ambayo serikali  imewafanyia na kuomba Rais Magufuli awe rais kwa awamu nyingine ya miaka mitano.

“Vijana tulikuwa na changamnoto ya ajira kwa kujenga viwanda ambapo huo unakuwa muarubaini wa tatizo la ajira, amefungua mradi wa kuzalisha umeme ambapo utapunguza gharama za umeme na kumuondolea adha mwananchi kwa kulipa gharama kubwa ya umeme na wawekezaji wataongezeka,” alisema Maganza.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post